https://tpc.googlesyndication.com/simgad/8045142562622600543


Recent Post

Thursday, February 04, 2016

Bondia Mada Maugo na Abdallah Pazi kuparuana Sikukuu ya Pasaka

Mabondia Mada Maugo kushoto na Abdallah Pazi wakitunishiana misuli baada ya kusaini mkataba wa kuzipiga siku ya Sikukuu ya Pasaka katika Ukumbi wa Uwanja wa Ndani wa Taifa, Dar es salaam. Mratibu wa mpambano huo ni kocha wa mchezo wa masumbwi nchini Rajabu Mhamila 'Super D'.
Na Mwandishi Wetu
MABONDIA Mada Maugo na Abdalla Pazi 'Dulla Mbabe' wamesaini mkataba wa kuzipiga siku ya Sikukuu ya Pasaka katika Uwanja wa Ndani wa  Taifa, ukiwa ni mpambano wa raundi nane KG 76.
Akizungumza wakati wa kutiliana saini mkataba huo, kocha wa mchezo wa masumbwi nchini ambaye ni mratibu wa mpambano huo amesema kuwa amewasainisha mabondia hao wanaotamba katika mchezo wa masumbwi nchini.
Mratibu wa mpambano wa masumbwi Rajabu Mhamila 'Super D' katikati akiwa na mabondia Mada Maugo kushoto na Abdallah Pazi wakati wa utambulisho wa mpambano wao utakaofanyika siku ya sikukuu ya Pasaka utakaofanyika  uwanja wa ndani wa Taifa.
Bondia Mada Maugo akikabiziwa mkataba wake na mratibu wa mapambano wa masumbwi  Rajabu Mhamila 'Super D' kati yake na Abdallah Pazi mpambano utakaofanyika siku ya sikukuu ya Pasaka  katika uwanja wa ndani wa Taifa.

Bondia Abdallah Pazi kushoto akipokea sehemu ya fedha yake kwa ajili ya maandalizi ya mpambano wake na Mada Maugo utakaofanyika uwanja wa ndani wa taifa anaetoa fedha hizo ni mratibu wa mpambano uho Rajabu Mhamila 'Super D'.



Bondia Abdallah Pazi kushoto akipokea mkataba wake kutoka kwa mratibu wa mpambano uho  Rajabu Mhamila 'Super D'  baada ya kusaini kwa ajili ya kupigana na Mada Maugo siku ya sikukuu ya Pasaka katika uwanja wa ndani wa Taifa.

 Bondia Mada Maugo kushoto akipokea sehemu ya malipo ya awali kutoka kwa mratibu  Rajabu Mhamila 'Super D' wa mpambano wake na Abdallaha Pazi. utakaofanyika siku ya sikukuu ya Pasaka.


Mbali na mpambano huo siku hiyo bondia chipkizi anaekuja kwa kasi zaidi katika mchezo wa masumbwi Vicent Mbilinyi anaetokea katika Super D  Boxing Promotion atapambana na Mwinyi Mzengela, mpambano wa KG 63 raundi nane huku bondia Cosmas Cheka na Mohamed Matumla wakionyeshana kazi na Pius Kazaula atakumbana na Seba Temba.

No comments:

LinkWithin

Related Posts Plugin for WordPress, Blogger...