https://tpc.googlesyndication.com/simgad/8045142562622600543


Recent Post

Friday, January 30, 2015

Wilaya ya Handeni lawamani tena, yalalamikiwa kutaka kubadili jina la Kwachaga bila kushirikishwa wananchi

Mzozo mzito umeibuka katika kijiji cha Kwachaga, Kata ya Kwachaga baada ya baadhi ya viongozi wa serikali ya Kata hiyo kupendekeza kubadilishwa jina la kijiji hicho kutoka Kwachaga na kuwa Turiani, huku Kwachaga ikiitwa kama Komkole. Uamuzi huo umeibua utata mkubwa ikiwa ni mwendelezo wa maamuzi yasiyoshirikisha wananchi wao.

Uamuzi huo unafanana kwa karibu na ule wa kuhamisha kijiji cha Misima, Kata ya Misima na kuingizwa kwenye Halmashauri ya Mji wa wilaya ya Handeni, mkoani Tanga, zaidi ikitumia pia jina la Mabanda badala ya Misima, Wadau mbaalimbali wa maendeleo ya Handeni wameanza kutoa maduku duku yao dhidi ya maamuzi hayo, huku gazeti la Majira la Januari 30 likiwa limeandika kwa kirefu kadhia hiyo ilipoanzia hadi ilipofikia wakati huu.


No comments:

LinkWithin

Related Posts Plugin for WordPress, Blogger...