https://tpc.googlesyndication.com/simgad/8045142562622600543


Recent Post

Saturday, January 31, 2015

Maonyesho ya Tanzania Buildex Internatinal Trade Exhibition kufikia tamati leo Januari 31

Na Andrew Chal, Dar es Salaam
MAONYESHO ya Tanzania Buildex Internatinal Trade Exhibition January 29 -31, yanayoendelea ndani ya ukumbi wa mikutano wa Mlimani City Conference, yanatarajia kufikia tamati jioni ya leo.
Direct Sales Agent wa SimbaNET, Lilian Godfrey (kushoto) akiwa na Deusdedit Msafiri  wa SimbaNET, wakiwa kwenye maonesho ya Tanzania Buildex Internatinal Trade Exhibition, Mlimani City.
Maonyesho hayo yaliyoandaliwa na kampuni ya  kigeni kutoka falme za kiarabu  ya S.K.M Air Conditioning LLC na wadau wengine yameshirikisha makampuni zaidi ya 50, ya ndani na nje ya Tanzania ambapo wameonyesha bidhaa zao hizo pamoja na kuuza.

Baadhi ya makampuni yaliyoshiriki kwenye maonesho hayo ni pamoja na kampuni ya huduma za internet ya Simba Net (T) LTD, TRADEX  Corporation, Choice International wasambazaji wa bidhaa za Lontor, ISTSL Limited, Rehoboth, Fairy Delights,  Afri Vision, Dello Enterprises Ltd wasambazaji wa vifaa vya SKF, SATA Ltd, na mengine mengi.

Makampuni hayo ni yale ya bidhaa za ujenzi, vifaa vya magari, vitu vya ndani, bidhaa za viwandani, maofisini na sehemu mbalimbali pamoja na makampuni ya bidhaa tofautitofauti.

No comments:

LinkWithin

Related Posts Plugin for WordPress, Blogger...