https://tpc.googlesyndication.com/simgad/8045142562622600543


Recent Post

Saturday, October 01, 2011

Meneja wa Sinta amwaga sera


MENEJA wa msanii wa filamu aliyewahi kutamba mno miaka ya nyuma, Christina Manongi, Richard Methew, amesema filamu itakayowakutanisha mwanadada huyo na Juma Kassim maarufu kama ‘Juma Nature’, itakuwa moto wa kuotea mbali, endapo makubaliano yao yatafikiwa na wawili hao.

Kwa siku kadhaa sasa wawili hao wamekuwa wakikutanishwa kwa nia ya kupatanishwa ili wacheze filamu hiyo, baada ya kuingia kwenye malumbano, yaliyosababisha Juma Nature atunge vibao viwili vya ‘Sitaki Demu’ na ‘Inaniuma Sana’.

Akizungumza jijini Dar es Salaam jana, Methew alisema hadi sasa Sinta bado hajakuwa tayari, licha ya kuonekana kuelekea kwenye makubaliano hayo.

Alisema mara baada ya kufikia makubaliano yao, wawili hao watacheza filamu hiyo na kutangazwa kwa wadau kwa nia ya kuona kazi yao inakuwa nzuri.

“Nimejaribu kuangalia vipi Sinta anaweza kurudi kwenye sanaa yake, huku nikiamini kuwa akicheza na Nature inaweza kuwa kazi nzuri zaidi na kumrudisha kileleni.

“Najivunia kuwa na msanii kama Sinta, hivyo naamini akifikia makubaliano kwa kusahau yote yaliyopita, mambo yanaweza kuwa mazuri zaidi,” alisema Mathew.

Hata hivyo, Sinta alipozungumza na Gazeti hili jana, alisema hana nia ya kurudi kwenye uhusiano wa kimapenzi na Juma Nature, hivyo wadau wanapaswa kuelewa katika hilo.



                                 Juma Nature chini na Sinta juu.  
Mwanadada huyo ni miongoni mwa wasanii wa kike mahiri na wanaosubiriwa kwa hamu kubwa katika ulingo wa filamu, huku umbo na sura yake likichanganya wengi, tangu wakati huo anashiriki katika michezo ya kundi la Kaole Sanaa Group.

No comments:

LinkWithin

Related Posts Plugin for WordPress, Blogger...