https://tpc.googlesyndication.com/simgad/8045142562622600543


Recent Post

Tuesday, December 30, 2014

Moto mkubwa wazuka Handeni Mjini muda huu baada ya gari la mafuta kugonga nguzo ya umeme



HABARI za kusikitisha ni kwamba moto mkubwa unaendelea kuwaka Handeni Mjini, mkoani Tanga, baada ya gari la mafuta kuanguka kufuatia kugonga nguzo ya umeme na kumwaga mafuta.

Ajali hiyo imesababisha kuwaka kwa moto mkali ambao unatajwa kuweza kuleta athari kubwa, hasa kutokana na eneo lililowaka moto huo.

Taarifa kutoka kwa mashuhuda wa ajali hiyo aliyejitambulisha kwa jina la Pedeshee Kunguru zinasema kuwa juhudi za kuuzima moto huo zimechelewa kutokana na jeshi la polisi kuchelewa kufika.

Alipotafutwa Mkuu wa Polisi wilayani Handeni, OCD Tindwa, mwandishi wetu hajaweza kuelewana naye kutokana na simu yake kupokewa huku akiwa kwenye kelele nyingi.

Juhudi za taarifa kamili ya moto huo zinaendelea kusakwa na mwandishi wetu aliyopo ndani ya Handeni, akishuhudia kila kinachojiri katika ajali hiyo.

Kwa taarifa za awali, moto huo umewaka kutoka katika barabara ya Songe, karibu na duka kubwa la mtu aliyetambuliwa kwa jina la John Shayo, huku ukishuka katika maeneo yenye hoteli.

 

No comments:

LinkWithin

Related Posts Plugin for WordPress, Blogger...