https://tpc.googlesyndication.com/simgad/8045142562622600543


Recent Post

Friday, April 06, 2018

Muriya: Makazi yetu Oman ni fursa za kiuchumi kwa watu wote

Makazi ya Jebel Sifah nchini Oman ni fursa za kiuchumi kwa watu wote

Balozi Mdogo wa Oman Visiwani Zanzibar, Ahmad Mohamed Al Muzaini wa nne kutoka kulia akiwa amesimama baada ya kumaliza kuzungumza kwenye maonyesho ya makazi ya Oman Visiwani Zanzibar yakiandaliwa na Kampuni ya Muriya yenye maskani yake nchini Oman. Maonyesho hayo yamefanyika katika Hoteli ya The Park Hyatt, Zanzibar. Wengine ni wadau wa ardhi na makazi waliohudhuria kwenye maonyesho hayo. Picha na Mpiga picha wetu.

Na Mwandishi Wetu, Zanzibar
HUKU maonyesho ya makazi ya Jebel Sifah yanayoonyeshwa na Kampuni ya Muriya yenye maskani yake nchini Oman yakiendelea visiwani Zanzibar katika Hotel ya The Park Hyatt, baada ya kumalizika jijini Dar es Salaam, wafanyabiashara wa visiwani hapa wametakiwa kupanua wigo wao wa kibiashara kwa kununua makazi yao nchini Oman ili wajiwekee vitega uchumi kwa ajili ya maendeleo yao.

Ushauri huo umetolewa leo na Meneja Mauzo wa Muriya, Ghizlane El Gouchi, wakati wa kuelimisha wakazi na wananchi wa Zanzibar juu ya utendaji kazi wao katika sekta ya ardhi na makazi waliyojikita nchini Oman, huku wakijivunia maendeleo makubwa kwenye sekta hiyo muhimu dunian kote.
Wadau wa ardhi na makazi nchini Tanzania, Ali Al Maskary kulia na Aflah Al Maskary kushoto wakifuatilia jambo na mdau wa ardhi kutoka Oman, Faisal Said Rashid Alzakwani katika maonyesho ya makazi yanayoendeshwa na kampuni ya Muriya yenye maskani yake nchini Oman kwa ajili ya kununua makazi nchini humo. Tukio hilo linafanyika leo Aprili 6, katika Hoteli ya The Park Hyatt, Zanzibar kuanzia saa nne asubuhi hadi saa moja jioni.
Faisal Said Rashid Alzakwani kushoto akipiga picha na aalozi mdogo wa Oman Visiwani Zanzibar, Ahmad Mohamed Al Muzaini.
Alisema kwamba ni vyema Watanzania wote wakiwamo wafanyabiashara wakaelewa umuhimu wa kujitanua kibiashara kwa kuangalia uanIshwaji wa biashara nje ya mipaka yao, huku Kampuni yao ikifungua milango kwa kuwauzia makazi kwa utaratibu mzuri na rahisi katika maeneo yenye solo kama vile pembeni mwa bahari ambako wanaweza kuyatumia kama fursa za kiuchumi bila kusahau hati ya kuishi nchini Oman.

Muriya ni kampuni kubwa iliyojikita katika utoaji wa huduma za makazi na utalii nchini Oman, ambao kwa wiki moja sasa wanaendelea na maonyesho yao ya kibiashara wakianzia jijini Dar es Salaam na visiwani Zanzibar kama njia ya kubadilishana mawazo na kuwajulisha Wazanzibar na Watanzania kwa ujumla juu ya biashara zao.

“Umuhimu wa biashara ni kupanuka kutoka eneo dogo kwenda eneo kubwa, hivyo ni lazima wadau wa Zanzibar kutafuta fursa nyingine hususan za kuwekeza nchini Oman katika eneo la makazi ambayo tutawauzia na wao watalipa kwa awamu ndani ya kipindi cha miaka miwili, tukiamini kuwa kwa wale wenye malengo wanaweza kufanikiwa, ambapo asilimia 10 zitalipwa baada ya kujisajili, huku gharama zetu zikianzia Dola 98,000 tu,"Alisema.

Kwa mujibu wa El Gouchi, mradi wao wa Jebel Sifah ni mwendo wa dakika 40 tu kutoka Muscat, karibu na ufukweni ambayo yana ukubwa hadi wa square meter 365,000, ukiwa ni mradi mkubwa unaowahusu Watanzania wote na ni fursa nzuri za uwekezaji.

Maonyesho hayo ya kibiashara ya makazi yanayouzwa na Kampuni ya Muriya, yamefanyika jijini Dar es Salaam kwa mafanikio makubwa tangu Aprili 3 hadi 5, ambapo kwa wakazi wa Zanzibar wenyewe wamefanikiwa kufikiwa na maonyesho hayo jana Aprili 6 katika Hoteli ya The Park Hyatt kwa ajili ya kuhakikisha kwamba wananchi wanakuwa na elimu juu ya umuhimu wa uwekezaji kwenye sekta ya makazi.


No comments:

LinkWithin

Related Posts Plugin for WordPress, Blogger...