https://tpc.googlesyndication.com/simgad/8045142562622600543


Recent Post

Monday, January 16, 2017

Mwandishi wa Habari za Michezo aliyefariki Zanzibar kuzikwa kwao Lushoto, Tanga

Mwandishi wa habari za Michezo wa Gazeti la Uhuru, Amina Athuman (pichani) amefariki Dunia jana asubuhi katika Hosptali ya Mnazi Mmoja mjini Zanziba alipokuwa amelazwa kwa matibabu.

Amina alilazwa Hospitalini hapo baada ya kuzidiwa (kushikwa na uchungu) kutokana na ujauzito na kukimbizwa kupata huduma katika hospitali hiyo ambpo alijifungua mtoto wa Kiume (Bahati mbaya) na yeye akaendelea kupatiwa matibabu hadi ulipomkuta umauti asubuhi ya leo.

Amina alikua mjini Zanziba kikazi alipokwenda kuripoti mashindano ya Kombe la Mapinduzi, ambapo alikuwa arejee jijini Dar es Salaam jana.

Kwa mujibu wa taarifa kutoka kwa familia, mwili wa marehemu utawasili leo jijini Dar es Salaam tayari kwa kuanza safari ya kuelekea wilayani Lushoto, mkoani Tanga kwa mazishi.

Mungu ilaze roho ya Marehemu Amina Athuman mahala pema peponi, Amina

No comments:

LinkWithin

Related Posts Plugin for WordPress, Blogger...