https://tpc.googlesyndication.com/simgad/8045142562622600543


Recent Post

Thursday, June 09, 2016

Watumishi hewa 170 wabainika mkoani Mbeya na kuleta hasara ya Sh 773,882,066

Na Mwandishi Wetu, Mbeya
Serikali Mkoa wa Mbeya imebaini watumishi hewa 170 kutokana na uhakiki ulifanywana timu ya vyombo vya dola iliyoundwa na Mkuu wa Mkoa mbeya tarehe 20 April mwaka huu na idadi ya watumishi hewa imesababisha hasara ya she 773,882,066.

Hayo amesema leo na Mkuu wa mkoa wa Mbeya alipokutana na waandishi wa habari kutangaza matokeo ya timu akiyoiunda kuhakiki watumishi hewa. Pamoja na hasara hiyo watumishi hewa 58 kati ya 170 wamekopa mikopo katika benki jumla ya shilingi 481,574,351

Serikali pamoja na kufanya uhakiki iliwataka watuhumiwa kurejesha fedha zote zi kikubwa katika akaunti na sh 65,058,542. Mkuu wa mkoa amewaagiza wakurugenzi kwa kushirikiana na vyombo vya dola kuwasaka popote walipo watumishi hewa na kuwachukulia hatua za kisheria.


Aidha amewaagiza wakurugenzi, maafisa utumishi na maafisa wa mfumo kuwajibika kwa kuendelea kulipa watumishi hewa. Kuanzia sasa kila afisa utumishi atawajibika kuwaondoa watumishi watoro pale wanapibainika na amewataka wakurugenzi kuwa na mpango endelevu wa kudhibiti watumishi hewa

No comments:

LinkWithin

Related Posts Plugin for WordPress, Blogger...