https://tpc.googlesyndication.com/simgad/8045142562622600543


Recent Post

Thursday, June 09, 2016

Kanisa la Sinza Christian Center latupiwa vyombo vyake nje

Picha zote na Fredy Njeje/ Blogs za Mikoa.
HALI ya sintofahamu imeibuka baada ya Kanisa la Sinza Christian Center lenye maskani yake Sinza, jijini Dar es Salaam kutupiwa vyombo vyake nje kwa madai ya kudaiwa deni la pango la jengo hilo jumla ya Sh Milioni 100.

Mmiliki wa jengo hilo anatajwa kuwa ni Prosper Rwendera, huku amri ya kutoa vyombo nje vya kanisa hilo ikitolewa na mahakama kwa madai kuwa upangaji huo ulikuwa na utata.

Alipotafutwa msemaji wa Kanisa ambaye ni Askofu anayedaiwa kuvamia jengo hilo, hakupatikana kuzungumzia sakata hilo na hata waumini wa kanisa hilo walipotafutwa walikataa kwa madai hawana mamlaka ya kuzungumzia lolote kuhusiana na sakata hilo.
Hili ni eneo la Kanisa Hilo.

Viti  vyote vikiwa vimetolewa nje
 Vyombo vya Muziki vikiwa nje
 Magari yakiwa yanatolewa nje
 Vitu vikiwa nje ya jengo hilo ambapo mpaka sasa kuna sinto fahamu vinapelekwa wapi.
 Vikombe nje.
 Wametoa vitu vyote.
Magodoro na vitanda vyote nje.   
 Baadhi ya Magari yaliyotolewa katika Jengo hilo ambapo hapo awali ilikuwa ni Kanisa.
Kushoto kwa mbali ni Mke wa Miiliki wa Jengo hilo Bi. Patricia Prosper akiendelea na majukumu huku pembeni vijana wakipata maelekezo ya kuendelea kutoa vitu.
 Picha zote na Fredy Njeje/ Blogs za Mikoa.

No comments:

LinkWithin

Related Posts Plugin for WordPress, Blogger...