https://tpc.googlesyndication.com/simgad/8045142562622600543


Recent Post

Wednesday, April 19, 2017

Mshindi wa Biko Milioni 10 apokea fedha zake na elimu NMB

Ofisa wa Benki ya NMB kushoto akimkabidhi kadi yake ya benki mshindi wa shindano la bahati nasibu ya Biko baada ya kushinda Sh Milioni 10 za shindano hilo nchini Tanzania. Anayeshuhudia kulia ni Meneja Masoko wa Biko, Goodhope Heaven. Makabidhiano hayo ya fedha na kadi ya benki kwa mshindi huyo yalifanyika Makao Makuu ya benki ya NMB kama sehemu ya kumuandaa mshindi wa Biko kuzitumia fedha zake kwa uangalifu ili zimnufaishe kiuchumi.

Na Mwandishi Wetu, Dar es Salaam
MSHINDI wa shindano la bahati nasibu ya Biko ‘Ijue Nguvu ya Buku’, Christopher Mgaya, jana amepokea fedha zake sambamba na kupewa elimu ya kifedha kutoka Benki ya NMB ambapo alifunguliwa akaunti ya kuhifadhia fedha hizo.

Mgaya alitangazwa mwishoni mwa wiki katika droo ya kwanza ya kumtafuta mshindi wa Sh Milioni 10, droo iliyochezeshwa na Balozi wa Biko Tanzania, Kajala Masanja akishirikiana na mwakilishi wa Bodi ya Michezo ya Kubahatisha Tanzania, Juhudi Ngolo, jijini Dar es Salaam.

Mshindi wa Sh Milioni 10 wa mchezo wa kubahatisha wa Biko, Christopher Mgaya, akisikiliza wakati Meneja Masoko wa Biko Tanzania, wachezeshaji wa bahati nasibu ya Ijue Nguvu ya Buku, Goodhope Heaven, wakati anafanya mazungumzo na waandishi wa habari, jijini Dar es Salaam. Fedha hizo alikabidhiwa jana Makao Makuu ya NMB jijini Dar es Salaam sambamba na kupewa elimu ya kifedha ili fedha hizo zimnufaishe kiuchumi na kubadilisha maisha yake. 


Nia ya kufunguliwa akaunti katika tawi la NMB Makao Makuu jijini Dar es Salaam sambamba na kupatiwa elimu ya kifedha kwa mshindi huyo limetokana na kiu ya kumuandaa kijana huyo ili aweze kuzitumia ipasavyo fedha zake kwa ajili ya kumuinua kiuchumi kutokana na uwapo wa mchezo wa bahati nasibu huo unaochezwa kwa kufanya miamala ya kifedha kwenye Tigo Pesa, Mpesa na Airtel Money.
Ofisa wa NMB akimkabidh mshindi wa Biko kadi yake ya ATM ya benki hiyo tayari kwa matumizi yake.

Mshindi wa Sh Milioni 10 wa mchezo wa kubahatisha wa Biko, Christopher Mgaya, akipokea fedha zake alizoshinda baada ya kutangazwa mwishoni mwa wiki na kukabidhiwa mapema jana Makao Makuu ya NMB jijini Dar es Salaam sambamba na kupewa elimu ya kifedha ili fedha hizo zimnufaishe kiuchumi na kubadilisha maisha yake. Kulia kwake ni Meneja Masoko wa Biko Goodhope Heaven.

Akizungumza katika ufunguzi wa akaunti ya mshindi wao huyo jana jijini Dar es Salaam, Meneja Masoko wa Biko, Goodhope Heaven, alisema kwa mshindi wao wa Sh Milioni 10 wameona wasimuache hivi hivi badala yake wakaamua kumfungulia akaunti NMB sanjari na kupatiwa elimu ya kifedha ili zimuendeleze kimaisha.

“Biko ushindi ni nje nje kwa kuwa lengo letu ni kuwafanya Watanzania wafanikiwe kimaisha kwa kuutumia vema mchezo wetu huu kwa kuingia kwenye kipengele cha lipa bili kwenye simu zao za Mpesa, Tigo Pesa na Airtel Money kisha kuingiza namba ya kampuni 505050 na kumalizia namba ya kumbukumbu ambayo ni 2456.

“Biko tunalipa kwa haraka kwa zawadi za papo kwa hapo kuanzia Sh 5000, 10,000, 20,000, 50,000, 100,000, 500,000 na sh Milioni moja, huku zawadi ya ushindi wa Sh Milioni 10 inayopatikana kwa kuchezeshwa droo kila mwisho wa wiki italipwa kwa njia ya hundi na kumuingizia fedha zake benki kama tulivyofanya kwa mshindi wetu Mgaya aliyeibuka na ushindi kutokea Manispaa ya Temeke jijini Dar es Salaam,” Alisema.

Naye Mgaya alisema kwamba anawashukuru Biko kwa kumpatia zawadi yake kwa haraka sambamba na kumpeleka NMB ili apatiwe elimu namna gani atazitumia fedha hizo ili zimuendeleze badala ya kuzitumia kwa matumizi yasiyokuwa ya lazima.

“Wakati nashiriki kucheza Biko sikutaraajia kama ningeshinda, lakini baada ya awali kushinda pia Sh 5000, nilihamasika na kuendelea kucheza ambapo Jumapili sikuamini baada ya kupigiwa simu na Kajala akinitaarifu kuwa nimeshinda Sh Milioni 10, ushindi ambao hakika utanitoa sehemu moja kwenda nyingine hususan kwa kukamilisha ujenzi wa nyumba.

“Nawashukuru Biko huku nikiwakumbusha Watanzania wenzangu kuchangamkia fursa ya bahati nasibu ya Biko kwa sababu haiitaji kujua lolote zaidi ya kucheza kwa njia ya ujumbe wa simu na kuingiza miamala kiasi cha Sh 1000 na kuendelea, huku kila Sh 1000 tunayolipa ikitupatia nafasi mbili, zawadi za papo kwa hapo pamoja na nafasi ya kuingia moja kwa moja kwenye droo ya kubwa ya wiki yakuwania Sh Milioni 10,” Alisema Mgaya.

Bahati nasibu ya Biko imeanza kwa kasi kubwa nchini Tanzania, ambapo mbali na kumpatia zawadi yake ya Sh Milioni 10 mshindi wao, pia inaendelea kulipa fedha mbalimbali walizoshinda washiriki wao kwa haraka hali inayoongeza msisimko mkubwa kwa washiriki na Watanzania kwa ujumla.

No comments:

LinkWithin

Related Posts Plugin for WordPress, Blogger...