https://tpc.googlesyndication.com/simgad/8045142562622600543


Recent Post

Friday, September 21, 2012

Ukiona uchafu, huwezi kumuenzi mwenzi wako






MAMBO FULANI MUHIMU



Na Kambi Mbwana, Dodoma
MAPENZI ni jambo ambalo linaleta hisia mbili tofauti. Mosi; mapenzi yanaweza kukufanya uishi kwa raha kama mfalme. Pili, mapenzi hayo yakibadilika hukufanya uwe kama chizi.

Jambo hilo zuri linalofananishwa na sukari kwa yaliyowakalia vizuri, hubadilika na kuwafanya baadhi yao waone ugumu wa kuendelea kuishi, maana wanaowapenda wanawasumbua kwa kiasi kikubwa.

Ni kutokana na hilo, jamii inashauriwa kuwa makini katika suala hilo. Wasijaribu kukurupuka na kuchukua uamuzi wenye mashaka kwa namna moja ama nyingine, maana vinginevyo watatamani kujinyonga.

                                                     Kambi Mbwana


Hata hivyo, pamoja na yote hayo, lakini inajulikana wazi wazi kuwa dawa kubwa katika uhusiano wa kimapenzi ni kumfikisha mwenzako, kumuweka katika kilele cha ubora katika ulimwengu wa mapenzi.

Katu usiangalie umbo lako, sura yako katika kujigamba kwamba unaweza kupendwa na yoyote, wakati ni mzigo kitandani. Kama huna ujuzi katika suala la mapenzi, ondoa kupendwa, kuhitajiwa au kugandwa na yoyote.

Zaidi ya hapo, wachache wao watakupitia na kuchukua hamsini zao, maana huna ujanja wa kumuweka mwenzako katika furaha. Hivyo basi, ili jamii iwe kwenye ramani nzuri na furaha ya mapenzi, lazima tuwajulie watu wetu.

Tufahamu namna ya kuwachanganya kisaikolojia, bila kuangalia uzuri wetu, fedha zetu, maana hizo haziwezi kufanya penzi liwe na amani.

Wapo ambao wanaishi na wanaume wenye nazo kupita kiasi, lakini bado wake zao, wachumba zao au wapenzi wao wanajiingiza katika uhusiano na watu wa kawaida, wakiwamo wafanyakazi wa ndani.

Hata hivyo haitoshi, wapo pia wakina mama wenye nazo lakini wanachanganywa na wasichana wa kawaida, wenye sura za kawaida au hadhi za kawaida. Wenye mali zao wanalia na kusaga meno.

Wanasema“Hivi kwani mume wangu unatembea na yule mfanyakazi wa ndani wakati mimi nipo” Au sielewi unachofuata kwa yule kijana mchunga mbuzi wakati mimi nipo, tena mwenye fedha za kutosha tu”

Kama wewe ni miongoni mwa watu wenye mtazamo huo umeliwa. Fedha sio kila kitu katika mapenzi. Fedha zako usipoangalia zinaweza kuwanufaisha wapita njia, wajuzi wa mambo kwenye mambo fulani muhimu.

Huo ndio ukweli wa mambo. Mjuzi huyo hatafutwi ili mradi mtu ana mtu wa nje, ila umuhimu wake unakuja anapokuwa kwenye ulingo. Hayo lazima mimi na wewe tuyajuwe kwa ajili ya mapenzi yetu.

Unapokuwa na mpenzi wako, mume au mke wako lazima ujuwe yupo na wewe kwa ajili ya kujenga maisha ya wawili. Ili mwenzako afurahie uwepo wako, hakikisha kuwa walau unatumia muda wako hata kama kidogo kumridisha kimapenzi.

Kwa wale ambao kwa miaka mingi wameishi na wapenzi wao bila kutumia ujuzi wao, waanze leo. Na wale wanaoingia kwenye uhusiano leo, pia wawaangalie watu wao, namna gani walivyo na wanastahili aina gani ya mapenzi.

Ninaposema mapenzi, sio yale ya kukaa pamoja, kutembea pamoja au kumpigia simu kila baada ya dakika kumi. Mapenzi, tendo la ndoa lenye ujazo mkubwa linalostawisha uhusiano wa wawili wapendanao.

Hivyo basi tuwe makini katika kazi hiyo. Tukitaka kuwapa raha kweli wenzetu lazima tuache kazi na kufanya kazi. Tendo la ndoa sio mchezo mdogo. Sio kama kuwasha njiti ya kibiriti mahala palipotulia.

Inahitaji kusumbua akili na kusumbua pia mwili wako. Sina maana kama nataka muda wote muwe kwenye tendo la ndoa, ila mnapotaka kufunja amri hiyo ya sita, basi mfikishe mwenzako kileleni.

Usimchezee chezee tu ukamuacha. Nimeamua kuandika mada haya maana nimepata malalamiko mengi kutoka kwa wanawake. Baadhi ya wasomaji wangu, wamenipasha kwamba waume zao ni watu wa kwenda raundi moja halafu wanaangalia ukutani.

Kwa bahati mbaya, watu hao wanapolala uzungu wa nne, wanakuwa wanawanyanyasa wenzao, kama unavyojua tena gari linapowaka. Hali hiyo inakera kiasi cha kutamani wapiti njia.

Haya nayasema kwa uchungu, maana usaliti mwingi huibuka kama wawili wapendanao hawaridhishani. Kama unaona huna ujuzi wa kumuweka katika kilele mwenzako, tafuta msaada kwa watu.

Kabla ya kuendelea, niseme tu kutokana na aina ya gazeti lako la Mtanzania, tunashindwa kuandika kiundani zaidi mada za mapenzi, badala yake tunakuwa wepesi kujibu maswali yenu kwa kupitia simu au barua pepe.

Tunafanya hivyo baada ya kugundua kwamba watoto wengi nao hujifunza kinachoandikwa kwenye gazeti, jambo linalonifanya niandike kwa kuficha au yale yasiyokuwa ya ndani zaidi.

Tukutane wiki ijayo.

0712 053949
0753 806087

Mwisho


No comments:

LinkWithin

Related Posts Plugin for WordPress, Blogger...