https://tpc.googlesyndication.com/simgad/8045142562622600543


Recent Post

Saturday, December 07, 2013

TFF yatuma salamu za rambirambi kuomboleza kifo cha mzee Nelson Mandela, Afrika Kusini

 
Shirikisho la Mpira wa Miguu Tanzania (TFF) limepokea kwa masikitiko kifo cha Rais wa zamani wa Afrika Kusini, Nelson Mandela kilichotokea jana (Desemba 5 mwaka huu) nchini humo.

Msiba huo ni mkubwa katika familia ya mpira wa miguu kwa Afrika Kusini, Afrika na Dunia kwa ujumla kutokana na mchango mkubwa wa Mzee Mandela katika mchezo huo.

Mzee Mandela anakumbukwa kwa mchango wake katika Fainali za Afrika (AFCON) zilizofanyika mwaka 1996 nchini Afrika Kusini na hata zile za Kombe la Dunia zilizofanyika nchini humo mwaka 2010.

TFF tunatoa pole kwa Rais wa Chama cha Mpira wa Miguu Afrika Kusini (SAFA), Danny Jordan, na wananchi wa Afrika Kusini na kuwataka kuwa na subira na uvumilivu katika kipindi hiki kigumu cha msiba huo mzito.

Mungu aiweke roho ya marehemu Mandela mahali pema peponi. Amina.

No comments:

LinkWithin

Related Posts Plugin for WordPress, Blogger...