https://tpc.googlesyndication.com/simgad/8045142562622600543


Recent Post

Friday, March 17, 2017

Rais Magufuli afuta agizo la vyeti vya Waziri Mwakyembe

Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Mhe. Dkt. John Pombe Magufuli akizungumza na Wanahabari Mkoani Dodoma kuhusiana na kufuta agizo lililotolewa jana na Waziri wa Katiba na Sheria kuhusu Wananchi wanaohitaji kufunga ndoa kuanzia mwezi Mei mwaka huu kuwa na vyeti vya kuzaliwa. Rais Mhe. Dkt. Magufuli ameagiza utaratibu wa awali uendelee kutumika kwasababu wananchi wengi wa Tanzania hawana vyeti, hivyo wangekosa haki hiyo ya kufunga ndoa. Kushoto kwake ni Mkuu wa Mkoa wa Dodoma Jordan Rugimbana. PICHA NA IKULU

Usambara Development yatoa msaada wa saruji wilayani Lushoto

 Wanafunzi wa shule ya secondari viti kata ya shume wilayani Lushoto wakipokea mifuko ya saruji yenye thamani ya shilingi laki tano kwa ajili ya ujenzi wa choo kutoka kwa taasisi ya USAMBARA DEVELOPMENT INITIATIVE (UDI) ikiwa ni katika kuchangia juhudi za Mh. Mbunge wa Mlalo mh. Rashid Shangazi za kuleta maendeleo jimboni hapo.
 Diwani wa kata ya Vuga wilayani Lushoto mh. Dhahabu jumaa akipokea miche ya miti kutoka kwa taasisi ya USAMBARA DEVELOPMENT INITIATIVE , ikiwa ni juhudi za kuendeleza na kutunza mazingira wilayani Lushoto, pichani anayekabidhi ni katibu Mkuu wa UDI DIckson shekivuli na naibu katibu Mkuu Frank shempemba.

LinkWithin

Related Posts Plugin for WordPress, Blogger...