Na Mwandishi Wetu, Ileje
TAASISI ya kifedha ya Bayport Financial Services inayojihusisha na mambo ya mikopo kwa watumishi wa wa umma na kampuni zilizoidhinishwa, mwishoni mwa wiki ilizindua tawi lake jipya la 80 wilayani Ileje, mkoani Mbeya, huku Mkuu wa wilaya hiyo, Rosemary Staki Senyamule, akiwataka wananchi wake kukopa kwa sababu maalum.

 Mkuu wa Wilaya ya Ileje, Mheshimiwa Rosemary Senyamule kulia, akionyeshwa nyaraka za ofisi ya Taasisi ya Kifedha ya Bayport Financial Services, inayojihusisha na mambo ya mikopo katika uzinduzi wa taasisi hiyo katika wilaya hiyo ya Ileje, mkoani Mbeya. Kushoto ni Meneja wa Kanda ya Nyanda za Juu Kusini, Alpha Akim. Uzinduzi huo ulifanyika mwishoni mwa wiki iliyopita na kuhudhuriwa na watu mbalimbali wilayani humo. Picha na Mpiga Picha Wetu.
Kufunguliwa kwa tawi hilo si kutainua uchumi wa wananchi wa Ileje watakaotumia fursa ya uwapo wa ofisi hiyo, bali pia kutarahisisha utoaji wa huduma wa taasisi hiyo ya Bayport nchini Tanzania.

Wageni mbalimbali wakiangalia shughuli za uzinduzi wa tawi jipya la taasisi ya kifedha ya Bayport Financial Services, wilayani Ileje, mkoani Mbeya, mwishoni mwa wiki iliyopita, ambapo mgeni rasmi alikuwa Mkuu wa wilaya hiyo, Rosemary Senyamule.

Akizungumza katika uzinduzi wa tawi hilo jipya, Mkuu huyo wa wilaya Ileje, Rosemary alisema kuwa wananchi wakiitumia fursa ya tawi hilo kutainua pia kiwango cha uchumi cha watu wake.

Baadhi ya wageni waalikwa wakisoma vipeperushi vya taasisi ya kifedha ya Bayport Financial Services, wilayani Ileje, mkoani Mbeya.
Alisema suala la mikopo ni jambo jema kutokana na uwezo mzuri unaoweza kuwaendeleza wananchi, wakiwamo watumishi wa umma na wafanyakazi wa kampuni zote zilizoidhinishwa, ambao kimsingi ni watu wanaotakiwa kuendelezwa kwa mambo mengi.