https://tpc.googlesyndication.com/simgad/8045142562622600543


Recent Post

Tuesday, October 21, 2014

SIWEZI KUVUMILIA:TFF mpya bado imesimama, haijaanza mwendo



Na Kambi Mbwana, Handeni

BADO nipo pembeni ya barabara kuangalia msafara wa safari ya mafanikio ya soka la Tanzania linaloratibiwa na Shirikisho la Soka nchini TFF, chini ya Rais wake Jamal Malinzi, aliyeingia kwa mbwembwe nyingi katika ofisi hizo.


Mtu ambaye siku moja baada ya kuingia madarakani alifanya mabadiliko makubwa kwa kumuondoa Katibu Mkuu wake Angetile Osiah pamoja na Mkurugenzi wa Ufundi Sunday Kayuni. Yalifuata pia mabadiliko mengine, ambayo baadhi yake yameshavurugika.


Kubwa ni lile la kutakiwa na Shirikisho la Mpira wa Miguu Duniani (FIFA) kurejea katika ofisi zao za zamani zilizokuwapo Karume, Ilala, jijini Dar es Salaam, badala ya PPF Tower kama walivyodhamiria na kusisitiza ndipo palipokuwa na hadhi ya TFF mpya.


Pia vurugiko jingine ni baada ya kusitisha kwa mkataba wa Mkurugenzi wao wa Sheria Evodius Mutawala. Ukiacha hayo, pia yapo matatizo lukuki ambayo kwa kiasi kikubwa yameonyesha kuwa safari ya TFF mpya ina mashaka.


Bado haijaanza. Wanaopaswa kuanza safari hiyo, akiwamo Malinzi mwenyewe bado hajajua anaotaka kusafiri nao, jambo linalonifanya nishindwe kuvumilia. Bado najiuliza, Tanzania tumedhamiria kweli kusonga mbele kimaendeleo ya mpira wa miguu au tunacheza shere?


Naona tumekuwa wapiga hadithi tu. Wengine tunajifunza namna bora ya kulaumu hataa pale tunaposhindwa kutimiza wajibu wetu. Tangu Malinzi aingie madarakani, sikutaka kusema lolote juu ya safari yake. Ukimya wangu sikutaka niwe miongoni mwa wanaolaumu mara kwa mara, ila w3akati mwingine mtu anashindwa kuvumilia.


Ndio hapo ninapopata hoja ya kumuuliza Malinzi, ni kweli una ndoto ya kukuza soka la Tanzania? Hii ni kwasabababu maneno yamekuwa mengi kuliko vitendo. Na panapokuwa na vitendo basi vinaonekana havina mashiko.


Bado akili zetu tumezielekeza kwenye mechi za kirafiki za Taifa Stars. Labda tunaamini mashabiki wanaweza kuingia kwa wingi, hivyo gharama za kambi kujilipa. Kama huo ni uongo, basi upo karibu kabisa na ukweli. Akili nyingine ipo kwa Simba na Yanga, ingawa tunajua kuwa bado hatuna mfumo unaowaibua vijana na watoto kutoka vijijini.


Ndio hapa tunapohitaji wana mkakati wa TFF wenye mipango kabambe kwa ajili ya kufanya mchakamchaka maeneo ya Tanzania kutafuta vipaji si kwa kuwachagua mmoja mmoja wakiwa wamekaa vijiweni, ila tuandaye ligi bora kuanzia ngazi ya Kata, wilaya na Mkoa ili tupate wachezaji wengi wenye vipaji ambao ndio uti wa mgongo wa soka letu.

Kinyume cha hapo tupiga soga, miaka isonge.

Tuonane wiki ijayo

Tamasha la Handeni Kwetu laomba sapoti ya wadhamini



Na Mwandishi Wetu, Handeni
WADAU wa mambo ya utamaduni yakiwamo mashirika, makampuni na watu mbalimbali wameombwa kujitokeza kuliwezesha tamasha la Handeni Kwetu 2014, lililopangwa kufanyika Desemba 13 mwaka huu wilayani Handeni, mkoani Tanga.

Mratibu Mkuu wa Tamasha la Handeni Kwetu, Kambi Mbwana, pichani.
Tamasha hilo linafanyika huku mwaka jana likiwezeshwa kwa kiasi kikubwa na Shirika la Mfuko wa Hifadhi ya Jamii (NSSF) kwa ushirikiano na wadau mbalimbali walioliwezesha tamasha hilo kwa mara ya kwanza katika Historia ya Mkoa wa Tanga.

Akizungumza mjini hapa, Mratibu Mkuu wa Tamasha hilo, Kambi Mbwana, alisema kuwa wadhamini wakijitokeza kwa wingi kutaongeza chachu ya maendeleo ya nchi, sanjari na sanaa ya utamaduni inayotakiwa kuungwa mkono na watu wengi.

Alisema kuwa kitendo cha wadhamini kuendelea kuliunga mkono Tamasha hilo kutachangia kwa kiasi kikubwa kuinua uchumi wa nchi pamoja na kutangaza utamaduni wa Mtanzania.

“Mwaka jana wadau wengi walijitokeza kuliwezesha tamasha la Handeni, wakiwamo NSSF, hivyo tunaomba msimu huu pia tuendelee kushirikiana kuliwezesha Tamasha la Handeni Kwetu litakalofanyika Desemba 13 mwaka huu, Handeni Mjini.

“Hadi wakati huu, walioonyesha nia ya kulisaidia tamasha la Handeni Kwetu 2014 ni pamoja na SmartMind & Partners iliyopo chini ya Anesa Co. Ltd kwa kupitia kitabu chao cha Ni Wakati wako wa Kung’aa, Phed Trans, chini ya Yusuphed Mhandeni, Handeni Kwetu Foundation, Wait & Watch Film Company Ltd, Qs Mhonda J Apex Group of Companies Ltd na Skyblue Security and Risk Mgt Ltd,” alisema Mbwana.

Tamasha la Handeni Kwetu ni miongoni mwa matukio makubwa ya kiburudani mkoani Tanga, ambako zaidi ya watu 500 walihudhuria tamasha hilo ambalo kwa mwaka huu mipango kabambe ya kuhakikisha kuwa linafanyika kwa mafanikio.


Monday, October 06, 2014

SIWEZI KUVUMILIA:TFF mpya bado imesimama, haijaanza mwendo


Na Kambi Mbwana, Dar es Salaam

BADO nipo pembeni ya barabara kuangalia msafara wa safari ya mafanikio ya soka la Tanzania linaloratibiwa na Shirikisho la Soka nchini TFF, chini ya Rais wake Jamal Malinzi, aliyeingia kwa mbwembwe nyingi katika ofisi hizo.


Mtu ambaye siku moja baada ya kuingia madarakani alifanya mabadiliko makubwa kwa kumuondoa Katibu Mkuu wake Angetile Osiah pamoja na Mkurugenzi wa Ufundi Sunday Kayuni. Yalifuata pia mabadiliko mengine, ambayo baadhi yake yameshavurugika.


Kubwa ni lile la kutakiwa na Shirikisho la Mpira wa Miguu Duniani FIFA kurejea katika ofisi zao za zamani zilizokuwapo Karume, Ilala, jijini Dar es Salaam, badala ya PPF Tower kama walivyodhamiria na kusisitiza ndipo palipokuwa na hadhi ya TFF mpya.


Pia vurugiko jingine ni baada ya kusitisha kwa mkataba wa Mkurugenzi wao wa Sheria Evodius Mutawala. Ukiacha hayo, pia yapo matatizo lukuki ambayo kwa kiasi kikubwa yameonyesha kuwa safari ya TFF mpya ina mashaka.


Bado haijaanza. Wanaopaswa kuanza safari hiyo, akiwamo Malinzi mwenyewe bado hajajua anaotaka kusafiri nao, jambo linalonifanya nishindwe kuvumilia. Bado najiuliza, Tanzania tumedhamiria kweli kusonga mbele kimaendeleo ya mpira wa miguu au tunacheza shere?

Kitabu cha ‘Ni Wakati wako wa kung’aa’ chadhamini tamasha la Handeni Kwetu 2014



Na Mwandishi Wetu, Handeni
KAMPUNI ya SmartMind & Partners iliyopo chini ya Anesa Co. Ltd, imejitosa kudhamini tamasha la Handeni Kwetu 2014, litakalofanyika Desemba 13, wilayani Handeni, mkoani Tanga.

Kitabu cha Ni Wakati wako wa kung'aa kinavyoonekana kwa nje
Ni mara ya pili kwa kampuni hiyo kudhamini tamasha hilo, kwa kupitia Kitabu chao kijulikanacho kama ‘Ni wakati wako wa kung’aa’, kilichoandikwa na Albert Sanga.

Akizungumza jana mjini hapa, Mratibu Mkuu wa tamasha hilo, Kambi Mbwana, alisema kwamba kwa kudhamini tamasha hilo, kampuni hiyo itakuwa na haki zote za kuuza kitabu chao sambamba na kutangaza bidhaa zao kwa kupitia tamasha hilo.

Alisema Sanga ni mjasiriamali mzalendo na mdau wa maendeleo ya Tanzania, hivyo anaamini wadau wa tamasha hili na Watanzania wote wananufaika kwa kiasi kikubwa mno.

“Tunashukuru kwa kupokea taarifa nzuri za udhamini kutoka kwa SmartMind&Patners kwa kupitia kitabu chao cha Ni wakati wako wa kung’aa, kikiandikwa na Sanga, ambaye ndio Mkurugenzi Mtendaji wa kampuni hiyo.

“Mbali na hao, wengine walionyesha moyo wa kulisaidia tamasha hilo msimu huu kwa wakati huu ni pamoja na Phed Trans, chini ya Yusuphed Mhandeni, Handeni Kwetu Foundation, Wait & Watch Film Company Ltd, Qs Mhonda J Apex Group of Companies Ltd na Skyblue Security and Risk Mgt Ltd,” alisema.

Mbwana alimaliza kwa kuwataka wadhamini wengine kujitokeza kwa wingi yakiwamo mashirika na taasisi za kiserikali kuingia kwenye udhamini ili waliwezeshe tamasha hilo sambamba na kutangaza biashara zao.

Saturday, October 04, 2014

Wait & Watch kutoka na filamu ya ‘Lifti’

Na Mwandishi Wetu, Dar es Salaam
KAMPUNI inayokwenda kwa jina la Wait & Watch Film Company Ltd, ipo mbioni kukamilisha filamu yake ya kwanza itakayojulikana kama ‘Lifti’ inayotengenezwa kwa umakini wa hali ya juu.
Adam Mchomvu, mmoja  ya wasanii walioshiriki katika filamu ijulikanayo kwa jina la Lifti.

Filamu hiyo itakuwa ya kwanza tangu kampuni hiyo iliposajiliwa kwa ajili ya kujihusisha na kazi mbalimbali za sanaa, ikiwamo filamu hapa nchini, huku ikiwa na mipango lukuki.

Akizungumza leo asubuhi, jijini Dar es Salaam, Mkurugenzi wa Kampuni hiyo, Athuman Kilo, maarufu kama 'Dr Kilo' alisema kuwa wamejipanga imara kuteka soko la filamu hapa nchini.

Alisema mashabiki wa filamu watapata burudani kamili pamoja na kujifunza kutoka kwenye filamu hiyo ambayo kwa kiasi kikubwa inaandaliwa kwa utulivu wa hali ya juu.

“Hii ni kazi ya kwanza ambayo tunaamini itaanza vyema kwasababu vichwa vimetulia na kuangalia namna gani akili zetu zinafanikisha kutoa kazi nzuri.

“Naomba wadau wote wakae mkao wa kula kuisubiri filamu hii ambayo kwa sasa ipo katika hatua za mwisho kabisa kukamilika na itakuwa moto wa kuotea mbali,” alisema Dr Kilo.

Baadhi ya watu walioshiriki katika filamu hiyo ni pamoja na Adam Mchomvu, Khamis Said, Sudi Ally ‘Akui’, Sadiki Manyeko, Jazzmin, Tatu Kingwande, Mzee Jengua na wengineo.

LinkWithin

Related Posts Plugin for WordPress, Blogger...